Soggetto 1: Rinasce d'acqua e di Spirito
1-16. Upi ni mshahara wa dhambi?
Mshahara wa dhambi ni mauti. Haijalishi ni dhambi ipi au ya namna gani, kila dhambi itahukumiwa mbele ya Mungu, na hukumu ya kila dhambi ni kifo. Ili tuweze kupata upatanisho wa dhambi, watu wa Israeli iliwapasa kutoa kondoo asiye na doa mbele ya Mungu. Lakini aina hii ya sadaka haikuweza kwa namna Fulani kutakasa dhambi zote kwa wakati wote, “maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi” (Waebrania 10:4).
Kwa hiyo, Mungu alitayarisha sadaka ya Kondoo kukomboa watu toka dhambini. Kila mnyama wa sadaka alipaswa kuwekewa mikono kuweza kubeba dhambi zote na kufa badala yao.
Katika Agano Jipya, Yesu alichukua dhambi zote kwa kupitia ubatizo wake katika mto Yordani akiwa ni Mwanakondoo wa Mungu na kufa kwa ajili yetu. “Mshahara wa dhambi ni mauti bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu” (Warumi 6:23).
Mshahara wa dhambi ni mauti, lakini Yesu alionyesha upendo wake kwa kufa badala yetu na kutuletea zawadi ya uzima wa milele kwa sisi wale tulio wenye dhambi ulimwenguni.
- Prima
1-32. Poiché Dio è grazioso e compassionevole, non ci considererebbe giusti, anche se nel nostro cuore c’è peccato, se crediamo semplicemente in Gesù?
- Dopo
1-33. Se diciamo che Gesù ha già eliminato tutti i nostri peccati del passato, del presente e del futuro secondo la tua affermazione, come si svilupperebbe il futuro di una persona se continuasse a peccare, pensando al fatto che ha già ottenuto il perdono dei suoi peccati credendo nel battesimo di Gesù e nella Croce? Anche se questa persona uccidesse un’altra persona, penserebbe che anche questo tipo di peccato gli sia stato espiato attraverso Gesù. Pertanto, continuerà a peccare senza esitazione, credendo semplicemente che Gesù abbia già eliminato anche i peccati che commetterà in futuro. Per favore, spiegami queste cose.