Search

Mahubiri

Somo la 10: Ufunuo (Ufafanuzi juu ya Ufunuo)

[23] Maswali & Majibu

1) Je, namba 144,000 katika sura ya 7 ina maanisha kiuhalisia juu ya watu wa Israeli ambao wataokolewa, au ni namba katika lugha ya picha? 
 
Namba 144,000 inayoonekana katika sura ya 7 inatueleza kiuhalisia kwamba ni Waisraeli wangapi ambao wataokolewa katika nyakati za mwisho, watu 12,000 toka katika kila kabila katika makabila kumi na mbili ya Israeli kwa ujumla wa 144,000. Hata yatatimizwa kwa majaliwa maalumu ya Mungu ambapo baadhi ya wana wa Ibrahimu, ambao Mungu aliwapaenda, wataokolewa. Mungu aliikumbuka ahadi aliyoifanya kwa Ibrahimu, hivyo ili kuitimiza ahadi hii, sasa ameiruhusu injili ya maji na Roho kuenezwa sio tu kwa wamataifa, bali pia kwa watu wa Israeli, ambao ni wana wa kimwili wa Ibrahimu. 
Kwa hiyo, Mungu ameazimia kwamba kwa kupitia dhiki ya nyakati za mwisho na kwa kupitia mashahidi wawili ambao Mungu atawainua kipekee kabisa kabisa kwa ajili ya Waisraeli, basi hapo ndipo Waisraeli watakapofikia hatua ya kumwamini Yesu Kristo, ambaye walimtesa na kumsulubisha, ndipo watatambua kwa hakika kuwa ni Mwokozi wao wa kweli. Waisraeli wamefanyika kuwa wapokeaji wa upendo maalumu wa Mungu kwa kupitia Mungu na imani ya Ibrahimu. 
Mungu ameamua kwamba atawakomboa watu 12,000 toka katika kila kabila ya Israeli toka katika dhambi zao na maangamizi, na kwa sababu hiyo amewawekea muhuri ya Mungu kwa kupitia malaika wake. Hivyo, watu 144,000 kati ya watu wa Israeli wamepokea alama inayowaonyesha kuwa wamefanyika kuwa watu wa Mungu. Idadi hii inagawanyika sawa miongoni mwa kabila kumi na mbili za Israeli, hii ni kwa sababu upendo wa Mungu kwa Waisraeli haupo katika misingi ya upendeleo kwa kabila fulani, bali anawavika wote kwa neema ile ile inayowafanya kuwa watu wake. Ingawa kwa baadhi ya nyakati watu huruhusu hisia zao kutawala hukumu na maamuzi yao, ukweli ni kuwa Mungu hutenda katika mambo haya yote kwa haki kamilifu na usawa. 
Baada ya kuwawekea muhuri wa wokovu watu 144,000 wa Israeli, basi hapo ndipo Mungu atakapoyamimina mapigo makuu hapa duniani. Mungu amefanya jumla ya Waisraeli 144,000 kuwa watu wake, watu 12,000 toka katika makabila kumi na mbili ya Israeli—yaani kuanzia kabila la Yuda, Rubeni, Gadi, Asheri, Naftali, Manase, Simioni, Lawi, Isakari, Zabuloni, Yusufu, na Benyamini. Mungu amefanya hili kuitunza ahadi aliyomwapia Ibrahimu na wana wake kwamba atakuwa Mungu wao. 
Hivyo, Mungu ameamua kuwaokoa watu 144,000 wa Israeli. Hii namba 14 kama inavyoonekana katika Mathayo 1:17 ina maana maalumu kwetu, inatueleza kwamba Mungu ataianza kazi yake mpya miongoni mwa Waisraeli. Namba hii inajumuisha mapenzi ya Mungu kwamba sasa ataihitimisha historia ya ulimwengu wa kwanza hapa duniani na kisha kuwaruhusu Waisraeli waliookolewa kuishi katika Mbingu na Nchi Mpya.
Tunapoangalia mtiririko wa ukoo toka kwa Ibrahimu hadi kwa Yesu Kristo, tunaweza kuona kwamba kuanzia Ibrahimu hadi Daudi kuna vizazi 14, na kutoka Dauti hadi wakati wa kuchukuliwa utumwamini Babeli kuna vizazi vingine 14, na toka kuchukuliwa utumwani Babeli hadi kuzaliwa kwa Kristo kuna vizazi vingine 14. Kwa maneno mengine, tunaweza kuona kwamba Mungu anaanza kazi mpya kila baada ya vizazi 14. Mungu amewatia muhuri Waisraeli 144,000 kwa mapenzi yake kwamba atawafanya waishi maisha mapya, si katika ulimwengu wa sasa, bali katika Ufalme wa Mungu. Kama inavyoweza kuonekana, Mungu ni mwaminifu anayezitimiza ahadi zake alizowahi kumwahidi mwanadamu. 
 

2) Mashahidi Wawili Wanaoonekana Katika Sura ya 11 Ni Akina Nani? 
 
Mashahidi wawili wanaoonekana katika sura ya 11 ni watumishi wawili wa Mungu ambao Mungu atawainua kipekee ili kuwaokoa Waisraeli katika nyakati za mwisho. Ili kuitimiza ahadi yake aliyoifanya kwa Ibrahimu, basi Mungu atawafanya manabii hawa wawili, ambao wametumwa kuwakomboa Waisraeli toka katika dhambi, kufanya ishara na miujiza, na kisha kuwafanya Waisraeli huku wakiongozwa na wao kumrudia Yesu Kristo na kisha kumwamini Yesu kuwa Mwokozi wao. Hawa mashahidi wawili watawalisha Neno la Mungu watu wa Israeli kwa siku 1,260—yaani miaka mitatu na nusu ya kwanza katika ile miaka saba ya Dhiki Kuu. Kwa kuieneza injili ya maji na Roho kwa Waisraeli na kwa kuwafanya waiamini injili hii kwa kupitia mashahidi hawa wawili, basi hapo Mungu atawapatia Waisraeli wokovu ule ule ambao amewapatia Wamataifa, yaani ni kama vile Wamataifa walivyookolewa toka katika dhambi zao kwa imani. 
Ufunuo 11:4 inasema, “Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi.” Kuna mafafanuzi tofauti kuhusu mizeituni hiyo miwili; baadhi ya watu wanadiriki kusema kwamba wao ndio ile mizeituni miwili. Lakini mizeituni hii miwili inawamaanisha wale waliotiwa mafuta. Katika nyakati za Agano la Kale, mtu alitiwa mafuta wakati alipofanywa kuwa nabii, mfalme, au kuhani. Wakati mtu alipowekwa mafuta Roho Mtakatifu alishuka juu yake. Kwa hiyo, mti wa mzeituni una maanisha ni Yesu Kristo ambaye alitungwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu (Warumi 11:17).
Hata hivyo, tukiangalia Ufunuo 11:1—“Nikapewa mwanzi kama fimbo; na mmoja akaniambia, Inuka, ukalipime hekalu la Mungu, na madhabahu, na hao wasujuduo humo.”—tunapaswa kutambua kwamba lengo la sura ya 11 ni juu ya wokovu wa watu wa Israeli. Kwa maneno mengine, kuanzia wakati huo itaanza kazi ya kuieneza injili ya maji na Roho kwa Waisraeli, yaani juu ya ukombozi toka katika dhambi zao zote kwa kupitia neema ya wokovu iliyotolewa na Yesu Kristo, na kwa wao kufanyika watu wa Mungu wa kweli. Hivyo, mashahidi wawili ni manabii wawili wa Mungu ambao watainuka katika nyakati za mwisho ili kuwaokoa watu wa Israeli. 
Katika Biblia, kinara cha taa kina maanisha ni Kanisa la Mungu. Kwa hiyo, vinara viwili vya taa vina maanisha ni Kanisa la Mungu miongoni mwa Wamataifa na Kanisa lililoruhusiwa miongoni mwa Waisraeli. Mungu si Mungu wa Waisraeli tu, bali pia ni Mungu wa Wamataifa, kwa kuwa Yeye ni Mungu wa kila mtu. Kwa hiyo, Mungu amelianzisha Kanisa lake miongoni mwa Waisraeli na Wamataifa pia, na Mungu anafanya kazi ya kuziokoa nafsi za watu toka katika dhambi hadi siku ya mwisho kwa kupitia Kanisa lake. 
Kuanzia wakati wa Agano la Kale, Waisraeli walikuwa na manabii waliowekwa kwa Sheria ya Mungu, na kwa kupitia manabii hao Waisraeli walilisikia Neno la Mungu. Waisraeli wanayo Sheria ya Musa na Manabii. Kwa hiyo, wanafahamu kila kitu kuhusu utaratibu wa sadaka ya kuteketezwa na unabii wa Agano la Kale, na hii ndio sababu wanahitaji manabii wa Mungu waliochaguliwa toka katika watu wao wenyewe. 
Pia wanaamini kwamba wao ni watu wa Mungu waliochaguliwa, hivyo huwa hawazingatii wala kuwekea mkazo wanapoelezwa Neno la Mungu na Wamataifa. Hivyo, ni hadi pale manabii wanaoamini katika injili ya maji na Roho wanapokuwa wamechaguliwa na Mungu toka miongoni mwa Waisraeli, hapo ndipo Waisraeli wanapoweza kumkubali na kumwamini Yesu Kristo kuwa ni Mwokozi wao. 
Hii ndio sababu Mungu mwenyewe atawaleta manabii wawili toka katika watu wa Israeli na kisha kuwatuma kwa Waisraeli. Kwa kweli manabii hawa watafanya maajabu mengi ambayo watumishi wa Mungu wanaofahamika katika Angalo la Kale wameyafanya. Ufunuo 11:5-6 inatueleza kwamba, “Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa. Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo.” 
Pasipo hawa watumishi wa Mungu kuwa na nguvu na mamlaka kama hayo, watu wa Israeli wasingeliweza kutubu, hivyo Mungu atawavika mashahidi hawa wawili kwa nguvu zake. Mungu atawapatia mashahidi hawa wawili nguvu zake maalumu, ili waweze kulihubiri Neno la unabii kwa Waisraeli, na kuwashuhudia na kuwafanya waweze kuamini kwamba Yesu Kristo ndiye Masihi waliyemngojea kwa muda mrefu. Baada ya kuyaona maajabu yakifanywa na hawa mashahidi wawili, basi hapo ndipo Waisraeli watakapowasikia na kisha kumrudia Yesu Kristo. 
Baada ya mashahidi wawili kuikamilisha kazi yao ya kuieneza injili kwa Waisraeli, Mpinga Kristo atatokea katika ulimwengu huu, atasimama kinyume na kazi yao kuihubiri injili, kisha atawafanya wawe wafia-dini. Ufunuo 11:8 inatueleza kuwa, “Na mizoga yao itakuwa katika njia ya mji ule mkuu, uitwao kwa jinsi ya roho Sodoma, na Misri, tena ni hapo Bwana wao aliposulibiwa.” 
Baada ya kuwa wameihubiri injili kwa Waisraeli woe na hivyo kuitimiza kazi ya wito wao, mashahidi wawili watauawa mahali ambapo Yesu alisulubiwa hapo zamani. Ukweli huu unakazia ufafanuzi kwamba hawa mashahidi wawili ni kutoka miongoni mwa Waisraeli. Kwa kuwa wao ni watumishi wa Mungu wa watu wa Israeli. 
Kwa kuhitimisha, Mungu atawainua watumishi wake wawili ili kuwashuhudia Waisraeli, ambao wamekataa kumwamini Yesu Kristo, na ambao kiroho ni kama vile Sodoma na Misri, kwamba kwa hakika Yesu ni Masihi wao waliyemsubiri kwa muda mrefu, na kwa kupitia mashahidi hawa wawili waliovikwa nguvu za Mungu, basi Mungu atawafanya Waisraeli wamwamini Yesu. 
 

3) Mwanamke Katika Sura ya 12 Ni Nani? 
 
Mwanamke katika sura ya 12 ana maanisha ni Kanisa la Mungu katikati ya Dhiki Kuu. Kwa kupitia mwanamke anayeteswa na Mnyama, sura ya 12 inatuonyesha kwamba Kanisa la Mungu litadhuriwa sana na Shetani nyakati za mwisho zitakapowadia. Hata hivyo, kwa kupitia ulinzi maalumu wa Mungu, Kanisa la Mungu litamshinda Shetani na Mpinga Kristo kwa imani yake, kisha litapokea utukufu wa kuvikwa baraka kuu za Mungu. 
Kwa kuwa watakatifu wanaodumu katika Kanisa la Mungu watapokea maboresho ya imani hata katika nyakati za Dhiki, basi watamshinda Mpinga Kristo kwa kuyapokea mauaji ya kuwa wafia-dini kwa imani katika injili ya maji na Roho. Mungu anatueleza ukweli huu kwa kupitia lugha ya picha ya mwanamke katika sura ya 12. 
Ufunuo 12:13-17 inatueleza kwamba, “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume. Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo. Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule. Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake. Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.”
Shetani, ambaye mara nyingi katika Biblia anatajwa kuwa ni Mnyama, kwa asili yake alikuwa ni malaika aliyefukuzwa toka Mbinguni kwa kutaka kuchukua nafasi ya Mungu. Kwa kuwa kama matokeo ya uasi huo, Ibilisi, pamoja na malaika wengine waliomfuata walitupwa toka Mbinguni, na huku akifahamu kuwa hivi karibuni atafungwa katika shimo la kuzimu lisilo na mwisho, basi alikuja hapa duniani na kisha kulitesa Kanisa la Mungu na watakatifu wa Mungu. 
Ingawa Shetani alijaribu kumzuia Yesu Kristo asikifanye kile ambacho alikuja kukifanya hapa duniani—yaani kuwaokoa wanadamu toka katika dhambi—hata hivyo Kristo alizichukua dhambi za ulimwengu kwa ubatizo wake, akaimwaga damu yake Msalabani, akafufuka tena toka kwa wafu, na kwa sababu hiyo amewaokoa wanadamu toka katiak dhambi zao zote. Hivyo, Yesu aliyatimiza mapenzi ya Baba. Pamoja na Shetani kujaribu kuingilia kazi ya Yesu ya kuyatenda mapenzi ya Mungu ili kuwaokoa wanadamu toka katika dhambi, Kristo alizishinda vurugu za Ibilisi na akayatimiza mapenzi yote ya Baba. 
Hata hivyo, kwa kuwadanganya watu wengi na kuwafanya kuwa washirika wake, Shetani amewafanya wasimame kinyume na Yesu Kristo na kinyume na watakatifu. Hali akijua kuwa siku zake zinahesabika, anawashawishi watu wa hapa duniani kusimama kinyume na Mungu na anawatesa watakatifu. Kwa kuhakikisha kwamba ulimwengu unajawa na dhambi, Shetani amemfanya kila mtu kukimbilia dhambi na ameifanya mioyo yao kuwa migumu ili kusimama kinyume na Mungu kwa sababu ya maovu yao. 
Shetani anawashambulia watakatifu wapendwa wa Mungu kwa dhambi bila kikomo, kwa kuwa anafahamu kuwa ana muda mchache. Shetani amemfanya kila mtu katika ulimwengu huu kuikimbilia dhambi na ameifanya mioyo yao kuwa migumu ili kusimama kinyumena Mungu na watakatifu wa Mungu kwa dhambi zao. Kwa hiyo, nyakati za mwisho zitakapowadia, watakatifu ni lazima wailinde imani yao kwa kupambana na kumshinda Shetani. 
Lakini Mungu ameihifadhi baraka maalumu kwa ajili ya watakatifu wake, hii ni kwa sababu anawapenda watakatifu wanaodumu ndani ya Kanisa lake. Baraka hii ni kwamba atawatunza watakatifu kwa kuwajenga kiimani katika Kanisa la Mungu katika ile miaka mitatu na nusu ya kwanza katika ile miaka ya Dhiki, yaani kabla Mpinga Kristo hajatokea hapa ulimwenguni, na kisha kuwadanganya watu na kuwafanya kuwa watumishi wake ili kusimama kinyume na Mungu na watumishi wa Mungu. Kwa nini? Kwa sababu wakati wa dhambi nyingi utakapowadia na wakati Mpinga Kristo atakapotokea, basi ni lazima watakatifu watauawa na kuwa wafia-dini. Ili kufanya hivyo, Mungu atawatunza watakatifu wake kwa kupitia Kanisa lake na atawawezesha kuwa wafia-dini kwa imani yao kwa mika mitatu na nusu—yaani, “kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati” (Ufunuo 12:14).
 

4) Je, Babeli ni Nini? 
 
Neno Babeli linatumika katika Biblia kuumanisha ulimwengu huu ambao umeachana na Mungu. Habari kuhusu “Mnara wa Babeli” inapatikana katika Agano la Kale. Kadri watu walivyoziunganisha pamoja nguvu zao ili kuujenga Mnara wa Babeli ili kumwacha Mungu, Mungu aliwazuia ili wasiujenge mnara, aliharibu kazi yao kwa kuivuruga lugha yao, kisha akawatawanya. 
Vivyo hivyo, ulimwengu huu ni kama wakati wa Mnara wa Babeli. Wafalme wa nchi wamefanya ukahaba na wameishi kwa starehe kwa vitu hapa ulimwenguni, na wafanyabiashara wote wamemdharau Mungu katika maisha yao, wametingwa kwa kuuza na kununua vitu vyote ambavyo Mungu amewapatia. Kwa kutumia dini, manabii wa uongo wameishi maisha yao huku wakiongea kwa sauti, na kujibadilisha kuwa wafanya biashara wanaozifanyia biashara roho za watu, huku wakijirundia baraka ya utajiri wa mali na vitu vya ulimwengu huu. Wameupenda ulimwengu, huku wakisema hakuna ulimwengu uliojengwa na mwanadamu ambao umekuwa bora zaidi kuliko huu wa sasa. 
Vivyo hivyo, nyakati za mwisho zitakapowadia, ulimwengu huu utakuwa mchafu sana mbele za Mungu na dhambi itakuwa imeenea sana ndani yake kiasi kuwa Mungu hatakuwa na la kufanya zaidi ya kuuharibu ulimwengu huu ambao yeye mwenyewe aliuumba. Huku wakiupenda mno ulimwnegu, watu wa ulimwengu huu wameuhesabu ulimwengu huu kuwa ndio Mungu wao, huku wakiamini na kuufuata. Hivyo, ulimwengu huu umefanyika kuwa kitanda cha dhambi, watu wanaoishi katika kitanda hiki cha dhambi wamelewa kwa aina mbalimbali za dhambi, na hivyo dhambi hizi zimesababisha anguko la ulimwengu. Hivyo hatimaye ulimwengu utakabiliana na mwisho wake utakaoletwa na mapigo ya mabakuli saba ya Mungu. 
Sababu nyingine itakayofanya ulimwengu huu ukabiliane na mapigo ya mabakuli saba toka kwa Mungu ni kwa sababu, watu wake kwa vile wanavyoupenda ulimwengu, wamegeuka na kuwa watumishi wa Shetani na wa Mpinga Kristo, na huku wakiziunganisha juhudi zao na Mpinga Kristo, wamewaua watakatifu waliozaliwa tena upya wanaoamini katika injili ya maji na Roho iliyotolewa na Bwana. 
Nyakati za mwisho zitakapowadia, watu watasalimu amri kwa Mpinga Kristo, wataipokea alama ya Shetani itakayotolewa na Mpinga Kristo, na hivyo watageuka na kuwa watumishi wa huyo mwovu. Kwa kuwa watu wa ulimwengu huu, wakiwa wamefanya uhaini pamoja na Mpinga Kristo, watakuwa wamesimama kinyume na Mungu na kuwaua wataktifu wa Mungu, basi Mungu atawalipa sawasawa na walivyowaletea mateso, dhiki, na vifo kwa watakatifu. 
 

5) Ufalme wa Milenia Utaanza Lini? (Je, ni Ufalme Kabla ya Dhiki au Baada ya Dhiki?) 
 
Watu wengi wanaamini kwamba watakatifu watanyakuliwa kabla ya ujio wa Dhiki Kuu ya miaka saba, na kwamba wakati wa Dhiki Kuu watakuwa tayari wapo katika Ufalme wa Kristo wa Milenia, badala ya hapa duniani. Hata hivyo, tunapoithibitisha imani hii kwa Neno la Mungu, basi tunaweza kuona kwa urahisi kwamba imani hii si sahihi. 
Bwana Mungu wetu anautoa Ufalme wa Kristo kwa watakatifu wake kwa miaka elfu moja kama thawabu kwa ajili ya kufanya kazi na kuutoa uhai wao kwa ajili ya injili. Kama vile Ufunuo 20:4 inavyotueleza, “Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu.”
Kifungu hicho hapo juu kinatuelezea sisi ambao tutaweza kuingia katika Ufalme wa Milenia. Hawa ndio wale ambao pamoja na Dhiki Kuu, walipigana dhidi ya Mpinga Kristo, wakauawa ili kuilinda imani yao, wala hawakuipokea chapa ya Mnyama wala kuiabudu sanamu yake. Ili kutenganisha kati ya ngano na makapi, Mungu amewaruhusu wanadamu kuwa na chaguo la kuipokea au kutoipokea alama ya Mnyama. Mungu anataka kutenganisha ngano na makapi kwa kuwanyakua watakatifu na kisha kuwapa thawabu ya Ufalme wa Kristo kwa sababu ya imani na ushindi wao dhidi ya Shetani. 
Kwa kuwa watu wa Mungu watakuwa ndio kikwazo kikuu kwa Mpinga Kristo ili asisimame kinyume na Mungu, na kujifanyia sanamu yake, na ili asiweze kuwafanya watu kuipokea alama yake. Basi, Mpinga Kristo atazitoa juhudi zake zote ili kuwaondolea mbali. Lakini watakatifu hawatasalimu amri kwa yule Mnyama, watapambana naye kwa imani, watayapokea mauaji ya kuwa wafia-dini, na kwa sababu hiyo watamtukuza Mungu. Idadi kubwa ya watakatifu, huku wakiangalia zaidi juu ya maisha yao baada ya kifo, wayapokea kwa hiari mauaji ya kuwa wafia-dini ili kuilinda imani yao katika Mungu. Kwa kuwa Mpinga Kristo ataleta mateso mengi kiasi hicho kwa watakatifu katika kipindi cha Dhiki Kuu, basi ndio maana Mungu amemwandalia Mpinga Kristo na wafuasi wake mapigo ya mabakuli saba na adhabu ya kuzimu ambako wataungua milele. 
Kwa hiyo, ulimwengu huu utaangamizwa kikamilifu na utavunjwavunjwa kwa mapigo ya mabakuli saba, kwa tetemeko kuu, kwa kiasi ambacho hakijawahi kuonekana. Kama matokeo, ulimwengu wa kwanza utatoweka bila hata kuacha alama yake. Kisha Mungu atawaamuru malaika zake kumkamata Mnyama na kisha kumfunga katika shimo la kuzimu lisilo na mwisho kwa miaka elfu moja, Bwana wetu atamfunga kwanza Mnyama katika shimo la kuzimu kabla ya kuwaruhusu watakatifu wake kuishi katika Ufalme wa Kristo wa Milenia. 
Kwa kuwa shetani hatakuwepo katika Ufalme wa Milenia mahali ambapo watakatifu watatawala pamoja na Kristo, basi huko hakuna waongo wala laana tena. Isaya 35:8-10 inaelezea juu ya Ufalme wa Kristo ambao utawajia watakatifu walioshiriki katika ufufuo wa kwanza kama ifuatavyo: “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo. Hapo hapatakuwa na simba, wala mnyama mkali hatapanda juu yake; hawataonekana hapo; bali waliokombolewa watakwenda katika njia hiyo. Na hao waliokombolewa na Bwana watarudi, watafika Sayuni wakiimba; na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; nao watapata kicheko na furaha, huzuni na kuugua zitakimbia.”
Ufalme wa Kristo, utakaodumu kwa miaka elfu moja kama hapo juu, utakuja baada ya dunia kupitia Dhiki Kuu ya miaka saba na baada ya kupita na kuangamizwa kwa ulimwengu unaoongozwa na Shetani na Mpinga Kristo. Hivyo, ufalme huu, ni zawadi ambayo Bwana wetu atawapatia watakatifu wake kwa kuteswa na kuwa wafia-dini ili kuilinda imani yao katika injili ya maji na Roho, na kwa kufanya kazi ili kuihubiri injili hii. 
 

6) Mji wa Yerusalemu Mpya ni Kitu gani? 
 
Mji wa Yerusalemu Mpya ni Mji Mtakatifu katika Mbingu na Nchi Mpya ambayo Mungu amewaandalia watakatifu ambao watashiriki katika ufufuo wa kwanza. Baada ya kuyahitimisha mapigo ya mabakuli saba hapa duniani, Mungu atamfunga Shetani katika shimo la kuzimu lisilo na mwisho kwa miaka elfu moja, kisha atawapatia watakatifu walioshiriki katika ufufuo wa kwanza baraka ya kutawala milele pamoja na Bwana katika Ufalme wa Milenia, baada ya kuisha kwa miaka elfu moja, Mungu ataifanya mbingu na nchi ya kwanza kutoweka kisha atawapatia watakatifu zawadi ya Mbingu na Nchi Mpya. 
Wale ambao watazipokea baraka hizi ni watakatifu ambao wamepokea ondoleo la dhambi zao kwa kuamini katika injili takatifu ya maji na Roho iliyotolewa na Yesu Kristo. Bwana atafanyika kuwa Bwana-harusi wa watakatifu, na watakatifu watakuwa ni mabibi-harusi wa Mwana-kondoo ambaye amefanyika kuwa Bwana-harusi, watakatifu katika utukufu wakiwa wamevikwa ulinzi, baraka, na mamlaka ya Bwana-harusi katika Ufalme wake wenye utukufu. 
Mungu amewaandalia watakatifu hawa Mji Mtakatifu katika Mbingu na Nchi Mpya. Mji huu si mwingine bali ni Mji Mpya wa Yerusalemu. Mji huu umeandaliwa maalumu kwa watakatifu wa Mungu. Na mambo haya yote yamepangwa kwa watakatifu katika Yesu Kristo hata kabla Bwana Mungu hajauumba ulimwengu. Wale ambao kwa kuzitegemea nguvu za ajabu za Bwana Mungu, wataishi katika Ufalme wa Kristo wa Milenia basi hao wanastahilishwa kuingia katika Mbingu na Nchi Mpya ambapo Mji Mtakatifu unapatikana. 
Kuanzia wakati huu na kuendelea, watakatifu wataishi pamoja na Bwana milele katika Hekalu la Mungu. Kwa kuwa Mungu yupo pamoja nao, basi hakutakuwa na kifo tena, wala huzuni, wala kuomboleza, wala mateso, kwa kuwa mbingu na nchi ya kwanza vitakuwa vimepita, naye Mungu atafanya vitu vyote kuwa vipya. 
Mji wa Yerusalemu Mpya unang’ara, kwa kuwa una utukufu wa Mungu, na mwanga wake ni kama wa kito cha thamani, kama kito cha yakuti, kilicho angavu kama kioo. Hivyo, utukufu wa Mungu upo pamoja na mji na wale wote wanaoishi ndani yake. Mji una ukuta mkubwa na mrefu wenye milango kumi na mbili, milango mitatu kila upande; milango hii inalindwa na malaika kumi na mbili, na majina ya makabila kumi na mbili ya Israeli yameandikwa katika milango hiyo. Ukuta wa mji una misingi kumi na mbili, na juu yake yameandikwa majina ya mitume kumi na mbili wa Mwanakondo. 
Mji umewekwa kama mraba mkubwa, huku upande wake mmoja ukiwa na yadi 12,000—sawa na kilomita 2,220 (maili 1,390). Ukuta wake una dhiraa 144, ambazo ni takribani mita 72. Ukuta huu umejengwa kwa yakuti, na Mji ni wa dhahabu safi, kama vile kioo angavu. Misingi ya ukuta imepambwa kwa aina mbalimbali za vito vya thamani, na milango kumi na mbili ya mji imejengwa kwa lulu. 
Kwa kuwa Bwana Mungu na Mwana-kondoo wapo katika Mji, basi hakuna sababu ya mwanga wa jua wala mwezi. Pia mto wa maji ya uzima unatiririka toka katika kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-kondoo, huku ukiumwagilia Ufalme wa Mbinguni na kuvifanya vitu vyote kuwa vipya. Kila upande wa huo mto kuna mti wa uzima, unaozaa matunda kumi na mbili na kutoa matunda yake kila mwezi, na majani yake ni dawa ya kuwaponya mataifa. Katika mji huo hakuna tena laana, bali baraka za milele zinapatikana humo. 
 

7) Alama au Chapa ya Mnyama ni Kitu Gani? 
 
Wakati wa Dhiki Kuu, ili kumfanya kila mtu awe chini ya mamlaka yake, basi Mpinga Kristo atawalazimisha watu wote kuipokea alama au chapa yake katika mikono yao ya kuume au katika vipaji vya nyuso zao. Alama hii ni alama ya Mnyama. Mpinga Kristo atawataka watu kuipokea alama yake ili aweze kumfanya kila mtu kuwa mtumishi wake. Mpinga Kristo ataendelea na mipango yake ya kisiasa huku akitumia maisha ya watu kama nguvu yake. Ikiwa watu hawana alama inayoonyesha kuwa wao wapo upande wa Mnyama, basi atawazuia wasiweze kununua au kuuza chochote kile. Alama hii ni namba au jina la Mnyama. Wakati Mnyama atakapoonekana hapa ulimwenguni, watu walazimishwa kuipokea alama hii itakayokuwa imeundwa ama kwa jina lake au kwa namba yake. 
Ikihesabiwa, basi namba ya Mnyama katika alama hii ni 666. Hii ina maanisha kwamba Mnyama, ambaye ni Mpinga Kristo, anajitangaza kuwa yeye ni Mungu. Kwa maneno mengine, inaonyesha kiburi cha mwanadamu cha kujaribu kuwa kama Mungu. Kwa hiyo, yeyote atakayeipokea alama hii katika mkono wake wa kuume au katika kipaji cha uso wake atakuwa akimtumikia na kumwabudu Mpinga Kristo Mnyama kama ni Mungu. 
Wakati ulimwengu unapokabiliana na magumu mengi toka katika mapigo ya matarumbeta saba, Mpinga Kristo, hali akitiwa nguvu na Shetani, ataufanya ulimwengu wote kuwa chini ya utawala wake kwa nguvu kuu. Huku akijitibu jeraha lake la mauti na kufanya miujiza mingi ikiwemo kuleta moto toka angani, basi atawafanya watu wengi wa ulimwengu huu kumfuata. Kama vile mashujaa wanavyotokea wakati wa shida, Mpinga Kristo, mtu aliyepokea nguvu toka kwa Shetani, atayatatua matatizo magumu ambayo ulimwengu utakuwa ukikabiliana nayo kwa mamlaka makuu, na kwa sababu hiyo ataheshimiwa na watu wote wa ulimwengu kana kwamba ni Mungu. Kwa kuwa Shetani atawafanya watu wengi wamtumikie Mpinga Kristo kana kwamba ni Mungu, basi watu wengi wataishia kumwabudu kana kwamba ni Mungu. 
Hatimaye, Mpinga Kristo ataifanya kazi yake ya mwisho kwa msaada wa mnyama mwingine atakayetoka katika nchi. Mnyama wa pili atawalazimisha watu kutengeneza sanamu ya Mnyama, ambaye ni Mpinga Kristo; ataipatia sanamu hiyo pumzi kwa nguvu za Shetani na kuifanya iweze kuongea; na atamuua kila ambaye hataiabudu sanamu ya huyo Mnyama. Atamfanya kila mtu kuipokea alama au chapa ya huyu Mnyama katika mikono yao ya kuume au katika vipaji vya nyuso zao, na atamzuia yeyote yule asiye na alama hiyo kununua wala kuuza chochote. 
Kupokea alama ya Mnyama maana yake ni kusalimu amri na kuwa mtumishi wa mnyama huyo. Alama hiyo haitapokelewa kwa kulazimishwa kimwili, bali kwa kuwafanya watu wafanye maamuzi binafsi kuipokea. Lakini, kwa kuwa pasipo kuwa na alama hii hakuna anayeweza kukunua au kuuza kitu chochote kile, basi watu wote hapa ulimwenguni ambao hawajapokea ondoleo la dhambi watasimama upande wa Mnyama na wataishia kusalimu amri mbele zake. 
Hivyo, wale watakaosalimu amri kwa Mnyama na kisha kuipokea alama yake watatupwa pamoja na Ibilisi, katika ziwa liwakalo kwa moto na kibiriti. Wakristo wa mazoea ambao hawajazaliwa tena upya, na kwa kuwa mioyo yao haina Roho Mtakatifu, hatimaye watasalimu amri mbele ya Shetani, wataipokea alama katika mikono yao ya kuume au katika vipaji vya nyuso zao, kisha watamwabudu huyu Shetani kana kwamba ni Mungu. Wakati huo, ni wale tu waliopokea ondoleo la dhambi na walio na Roho Mtakatifu katika mioyo yao ndio watakaoweza kuyapinga matakwa ya kuipokea alama ya Mnyama, kisha watapambana na kumshinda Mpinga Kristo kwa imani. 
 

8) Viumbe Wanne Wenye Uhai Wanaosimama Mbele ya Kiti cha Enzi cha Mungu ni Akina Nani? 
 
Ufunuo 4:6-9 inaelezea juu ya viumbe wanne wenye uhai kama ifuatavyo: “Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na mfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, walikuwako wenye uhai wanne, wamejaa macho mbele na nyuma. Na huyo mwenye uhai wa kwanza alikuwa mfano wa simba; na mwenye uhai wa pili alikuwa mfano wa ndama; na mwenye uhai wa tatu alikuwa na uso kama uso wa mwanadamu; na mwenye uhai wa nne alikuwa mfano wa tai arukaye. Na hawa wenye uhai wanne, kila mmoja alikuwa na mabawa sita; na pande zote na ndani wamejaa macho, wala hawapumziki mchana wala usiku, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako na aliyeko na atakayekuja. Na hao wenye uhai wanapompa yeye aketiye juu ya kiti cha enzi utukufu, na heshima, na shukrani, yeye aliye hai hata milele na milele,…. ”
Wale viumbe wanne wenye uhai waliokizunguka kiti cha enzi cha Mungu, pamoja na wale wazee 24, ni watumishi waaminifu wa Mungu ambao wanaoyatenda mapenzi yake na kisha kuutukuza utakatifu wake na utukufu. Wakati Mungu anapotenda kazi, hatendi peke yake, bali anatenda wakati wote kupitia watumishi wake. Viumbe wanne wenye uhai, ni watumishi walio karibu zaidi na Mungu, wamepokea uwezo wa kuyatenda mapenzi ya Mungu wakati wote. 
Kila moja kati ya wale viumbe wanne wenye uhai ana umbo la peke yake, jambo linaloonyesha kwamba kila kiumbe hai anamtumikia Mungu kwa viwango tofauti. Viumbe hao wana macho pande zote ndani na nje, hii ina maanisha kwamba wakati wote wapo makini kuyaangalia madhumuni ya Mungu. Kwa hiyo, viumbe wanne wenye uhai ni watumishi waaminifu wa Mungu ambao wakati wote wanayatenda mapenzi yake. 
Kwa nyongeza, viumbe wanne wenye uhai hawapumziki katika kuusifu utukufu wa Mungu na utakatifu wake, ni kama vile Mungu asivyolala. Wanausifu utakatifu wa Mungu Baba na Bwana Yesu, ambaye ni Mwana-kondoo wa Mungu, pia wanazisifia nguvu zake kuu. Kwa namna hii, wale viumbe wanne wenye uhai wanaosimama mbele ya kiti cha Mungu cha enzi wanamsifu Mungu toka katika mioyo yao yenye unyenyekevu, na hawafanyi hivyo kama sehemu ya kulazimishwa. Kwa nini? Kwa sababu ya kile ambacho Yesu Kristo amekifanya—yaani, kwa kitendo chake cha kujishusha katika umbile la kibinadamu na kwa kuzaliwa hapa ulimwenguni kwa kupitia mwili wa Bikira Mariamu; kwa kuzichukua dhambi zote za mwanadamu katika mwili wake kwa kuupokea ubatizo toka kwa Yohana; kwa kuzichukua dhambi hizo hadi Msalabani na kisha kufa juu yake; na kisha kuwakomboa wanadamu toka katika dhambi—sasa, Yesu ameketi katika kiti cha enzi cha Mungu, na kwa sababu ya matendo haya mema anastahili kupokea utukufu toka kwa viumbe hawa wenye uhai milele na milele. 
Hivyo hawa viumbe wanne wenye uhai wakiwa pamoja na wazee 24 wanamwinua Mungu, kwa kumpatia sifa za kweli toka katika mioyo yao. 
 

9) Lipi ni Sahihi: Kunyakuliwa Kabla ya Dhiki, au Kunyakuliwa Baada ya Dhiki? Je, Watakatifu Watakuwepo Hapa Duniani Wakati wa Dhiki Kuu?
 
Tukiangalia historia ya Ukristo, tunaweza kuona kwamba idadi kubwa ya waongo wamekuwa wakiinuka hadi wakati huu wa sasa. Huku wakikifafanua Ktiabu cha Ufunuo na huku wakipigia hesabu muda wa unyakuo kwa kutumia mbinu yao binafsi, waongo hawa wamepanga tarehe maalumu ya unyakuo na wamekuwa wakifundisha kwamba Bwana atarudi na watakatifu watanyakuliwa siku hii ya kuchaguliwa kwao. 
Hata hivyo, madai hayo yote yaliishia kuwa ni uongo. Tabia moja ambayo inafanana sana miongoni mwao wote ni kwamba wanaitetea nadharia ya kunyakuliwa kabla ya dhiki. Wanawaeleza wafuasi wao kwamba mali walizo nazo hazitakuwa na maana yoyote ile kwa kuwa watanyakuliwa na kuinuliwa angani kabla ya Dhiki Kuu, hawa waongo waliwadanganya watu wengi na hivyo kuwaibia mali na vitu vyao. 
Tunapaswa kutambua kwamba hii ni mbinu ya Shetani, akijaribu kuwadanganya watu wote wa ulimwengu huu ili kuwageuza wawe wafuasi wake kwa kupitia uongo huu. 
Jambo muhimu zaidi kwa watakatifu, na jambo ambalo watakatifu wengi wanajiuliza, ni swali kwamba unyakuo wa watakatifu utatokea lini. Ufunuo 10:7 inatueleza kwamba, “isipokuwa katika siku za sauti ya malaika wa saba atakapokuwa tayari kupiga baragumu; hapo ndipo siri ya Mungu itakapotimizwa, kama alivyowahubiri watumishi wake hao manabii.” Je, aya hii inaposema kwamba, “siri ya Mungu itakapotimizwa” ina maanisha nini? “Siri ya Mungu” si kitu kingine bali ina maanisha ni unyakuo wa watakatifu. 
Baada ya mapigo sita kati yale mapigo ya matarumbeta saba ya Mungu kuisha, Mpinga Kristo atatokea hapa duniani, atautawala ulimwengu, na atamtaka kila mtu kuipokea alama ya Mnyama. Watakatifu watauawa na kuwa wafia-dini kutokana na mateso yake. Hii itafuatiwa mara na mlio wa tarumbeta la saba, ambapo watakatifu waliouawa kama wafia-dini pamoja watakatifu walio hai walioilinda imani yao watafufuliwa na kunyakuliwa. 
Wakati tarumbeta la saba litakapolia, Mungu hataleta pigo hapa duniani; bali, huu ni wakati ambapo unyakuo wa watakatifu utatokea. Baada ya unyakuo, basi Mungu ataendelea kuyamimina mapigo yake ya mabakuli saba hapa duniani. Kwa hiyo, kuwadia wakati wa mapigo ya mabakuli saba, watakatifu hawatakuwepo hapa duniani, bali watakuwa angani pamoja na Bwana. Sisi sote tunapaswa kutambua kwamba unyakuo wa watakatifu utakuja wakati malaika wa saba atakapolipiga tarumbeta la mwisho. 
Hata hivyo, hata sasa Wakristo wengi bado wanaendelea kuamini katika nadharia ya kunyakuliwa kabla ya dhiki. Kwa kuwa imani yao haijajiandaa kwa ujio wa majanga ya kiasili na kutokea kwa Mpinga Kristo, basi hatimaye watashindwa vita yao ya kiroho dhidi ya Shetani na Mpinga Kristo, watageuka na kuwa watumishi wake, kisha wataangamizwa pamoja na ulimwengu. 
Miaka mitatu na nusu ya kwanza katika ile miaka ya saba ya Dhiki Kuu ni wakati wa mapigo ya matarumbeta saba, wakati ambapo dunia itaharibiwa na majanga ya kiasili. Theluthi ya jua na theluthi ya nyota zitatiwa giza; theluthi ya misitu ya hapa duniani itaunguzwa; theluthi ya bahari itageuka na kuwa damu, huku ikiua theluthi ya viumbe hai ndani yake; vimwondo vitaanguka toka angani, na kuyageuza theluthi ya maji kuwa pakanga; na kama matokeo ya hayo, watu wengi sana watakufa. Ulimwengu utaangukia katika machafuko kutokana na mapigo haya, huku mataifa yakiinuka ili yapigane na mataifa mengine, huku falme zikipigana na falme, huku vita ikitokea sehemu mbalimbali. 
Kwa hiyo, wakati Mpinga Kristo atakapotokea na kuyatatua matatizo hayo yote katika hali yenye machafuko kama hiyo, basi watu wengi sana watamfuata, na kwa sababu hiyo watayaleta mapigo ya kutisha zaidi hapa duniani. 
Hivyo, ulimwengu huu utashuhudia kuinuka kwa asasi zenye mafungamano ya kisiasa ya kimataifa, utaratibu wa kiutawala ambao unashughulikia maslahi ya jumla ya mataifa yote. Muungano huu wa mataifa duniani utaangukia katika mikono ya Shetani huku Mpinga Kristo akitokea, kisha muungano huo utageuzwa kua ni muungano unaosimama kinyume na Mungu na watakatifu wake. Mtawala wa muungano huu wa kimataifa atayatawala mataifa yote, kisha atatenda kama Mpinga Kristo. Yeye, anayefanya kazi kwa kutumia nguvu za Shetani ni adui wa Mungu na ni mtumishi wa Ibilisi. 
Wakati huo, Mpinga Kristo atazionyesha rangi zake halisi, huku akiwazuia watu kutomwamini Mungu a kweli na kuwalazimisha wamwabudu yeye kana kwamba ni Mungu. Na ili kulitimiza hili, atafanya ishara nyingi mbele yao, atatatua matatizo mengi ya hapa ulimwenguni huku akitumia nguvu za Shetani, na kwa sababu hiyo ataukamata moyo wa kila mtu. 
Mwishoni, Mpinga Kristo atatengeneza sanamu yake na kuwataka watu wote waiabudu kana kwamba ni Mungu. Na ili kumweka kila mtu chini ya uongozi wake wakati huo wa dhiki, basi Mpinga Kristo atawalazimisha watu kuipokea alama yake katika mikono yao ya kulia au katika vipaji vya nyuso zao, na kisha atawazuia wote wasio na alama hii kufanya biashara yoyote ile. Pia atawaua wale wote ambao watakataa kumwabudu yeye, atawaua bila kujalisha idadi yao. Kwa hiyo, yeyote ambaye jina lake halijaandikwa katika Kitabu cha Uzima ataishia kuipoka alama hii na kisha kumwabudu Mnyama. 
Hata hivyo, watakatifu hawatasalimu amri kwa Mpinga Kristo wala kuipokea alama yake. Kwa kuwa Roho Mtakatifu anakaa katika mioyo yao, basi hakuna mwingine yeyote zaidi ya Mungu Mwenyezi wanayeweza kumwabudu kwa kuwa ni Bwana wao. Hivyo, watakatifu watakataa kumwabudu Shetani na Mpinga Kristo na kuwa watumishi wao, bali watauawa na kuwa wafia-dini kwa imani yao, na kwa sababu hiyo watawashinda Shetani na Mpinga Kristo. 
Kama vile Ufunuo 13:10 inavyotueleza, “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.” Wakati Mpinga Kristo atakapoonekana na kisha kuwalazimisha watu kuipokea alama yake, wakati huo miaka mitatu na nusu ya Dhiki Kuu itakuwa imeshapita, na kipindi cha miaka mingine mitatu na nusu kitakuwa kimeanza. Wakati huu watakatifu watateswa na Mpinga Kristo na kisha kuuawa kama wafia-dini. 
Lakini kitendo cha Mpinga Kristo kutwaa madarakana kuwatesa watakatifu ni mambo yaliyoruhusiwa na Mungu kwa kipindi cha muda mfupi tu, kwa kuwa Bwana atakifupisha kipindi cha Dhiki kwa watakatifu wake. Wakati huo, watakatifu watampatia Mungu utukufu kwa kupambana na Mpinga Kristo ili kuilinda imani yao na kisha kumshinda kwa wao kuwa wafia-dini. 
Baada ya kukipitia kipindi cha kwanza cha miaka mitatu na nusu katika ile miaka saba ya Dhiki Kuu, watakatifu waliozaliwa tena upya watakuwepo hapa duniani hadi watakapouawa na kuwa wafia-dini wakati ambapo kipindi cha pili dhiki kitakapokuwa kimeanza. Hivyo, watakatifu ni lazima wapambane na Shetani na Mpinga Kristo na kuwashinda kwa imani yao. Hii ndio sababu Ufunuo inatueleza kwamba Mungu atawapatia Mbingu wale watakaoshinda. Kwa hiyo, kabla ya kupita kwa miaka mitatu na nusu ya ile Dhiki Kuu na kabla ya kuonekana kwa Mpinga Kristo, basi imani ya watakatifu itatunzwa katika Kanisa la Mungu, yaani chini ya ulinzi na uongozi wa Bwana wetu. 
Hivyo, watu wanapaswa kuwekwa huru toka katika haya mafundisho mabaya ya kidini ambayo Shetani ameyaeneza katika jumuia za Kikristo, mafundisho hayo ni nadharia ya kunyakuliwa kabla ya dhiki, pia wanapaswa kupokea ondoleo la dhambi zao zote kwa kuamini katika injili ya maji na Roho na kisha kujiunga katika Kanisa la Mungu. Ni kwa kufanya hivyo tu ndipo imani yao inapoweza kujengwa kwa kupitia Kanisa la Mungu kwa miaka mitatu na nusu ya kwanza katika ile miaka ya Dhiki Kuu, na ni hapo ndipo wanapoweza kuwa imani inayoweza kupambana dhidi ya Mpinga Kristo na kisha kuyapokea mauaji yao wa kuwa wafia-dini utakapowadia wakati mgumu wa dhiki. 
 

10) Unaposema kwamba unyakuo utakuja baada ya malaika wa saba kulipiga tarumbeta lake, je, hujichanganyi kutokana na kile ambacho Bwana amekisema, kwamba hakuna mtu anayeijua siku wala saa ya unyakuo, akiwamo Bwana Mwenyewe? 
 
Hapana kabisa! Alichotueleza Bwana wetu si juu ya siku na saa ambapo watakatifu watanyakuliwa, bali ametueleza juu ya habari za utangulizi na ishara ambazo zitapelekea kutokea kwa tukio hili muhimu. Ni kwa kufahamu hivyo ndipo watakatifu wanaompenda Bwana wanapoweza kuiandaa imani yao, na hapo ndipo wanapoweza kushiriki katiak unyakuo kwa kupambana dhidi ya Mpinga Kristo na kuyapokea mauaji yao ya kuwa wafia-dini wakati utakapowadia. 
Kwa kupitia ufunuo wake, Mungu alimwonyesha Mtume Yohana, aliyekuwa uhamishoni katika Kisiwa cha Patmo mambo yote ambayo yatakuja kutokea nyakati za mwisho za ulimwengu huu. Vivyo hivyo, Mungu anapopanga na kuzitimiza kazi zake, basi huwa anahakikisha kuwa watumishi wake wanafahamu. 
Katika Neno la Mungu lote, Kitabu cha Ufunuo ndio kinachoongoza kwa kuandikwa kwa lugha ya picha. Kwa sababu hii, ni watumishi wa Mungu tu ambao wameokolewa toka katika dhambi zao zote kwa kuamini katika injili ya maji na Roho na hivyo kuwa na Roho Mtakatifu ndani ya mioyo yao ndio wanaoweza kuzielezea vizuri lugha hizo za picha kwa watu. Neno la Ufunuo linawafunulia kwa kina watumishi wa Mungu na watakatifu wake kuhusu mapigo ya matarumbeta saba, kuonekana kwa Mpinga Kristo, watakatifu kufia-dini, kufufuka na kunyakuliwa kwa wataktaifu, Ufalme wa Kristo wa Milenia, na Mbingu na Nchi Mpya. 
Kunyakuliwa kwa watakatifu kunahusiana kwa karibu kabisa na vifo vya wafia-dini. Ufunuo 11:10-12 inatueleza kuhusu kifo cha manabii wawili, na juu ya ufufuo na kunyakuliwa kwao kwa muda wa siku tatu na nusu. Mashahidi hawa wawili watauawa na Mpinga Kristo kisha baada ya siku tatu na nusu watafufuliwa toka mauti. Tunachoweza kukiona katika maelezo haya ni kwamba wakati Mpinga Kristo atakapoonekana hapa duniani na kisha kuwafanya watu wamwabudu Mnyama kwa kuipokea alama yake katika mikono yao ya kuume au katika vipaji vya nyuso zao, basi watakatifu watapambana dhidi ya Mpinga Kristo na kisha kuuawa na kuwa wafia-dini kwa imani yao, lakini kufuatia kurudi kwa Bwana muda mfupi baada ya kuuawa kwao na kuwa wafia-dini, watashiriki katika ufufuo wa kwanza na kisha kunyakuliwa. 
Pia Paulo alizungumzia juu ya unyakuo katika 1 Wathesalonike 4:16-17: “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.”
Wakati utawala wa Mpinga Kristo utakapoanza katika ulimwengu huu, wakati atakapojaribu kutulazimisha ili tuipokee alama yake, na wakati atakapodai aabudiwe kana kwamba ni Mungu, basi sisi watakatifu ni lazima tutambue kwamba wakati wa kuuawa kwetu na kuwa wafia-dini umewadia, pia ni lazima tuamini kwamba mara baada ya kuuawa kama wafia-dini utafuatia ufufuo na unyakuo wetu. Hatufahamu kuwa ni mwezi upi na ni siku ipi mambo haya yatatokea. Lakini tunachofahamu ni kwamba unyakuo wa watakatifu utakuja baada ya malaika wa saba kulipiga tarumbeta lake. Watakatifu wote ni lazima wajiandae kuipokea Siku ya Bwana kwa kuuamini ukweli huu. 
 

11) Unasema kwamba Yesu atakuja ili kuwanyakua watakatifu wake, na kwamba atashuka hapa duniani ili kupigana vita ya Harmagedoni. Je, una maanisha kwamba Bwana atakuja hapa duniani mara mbili? Je, tofauti ya mambo hayo mawili ni ipi? 
 
Kushuka kwa Yesu toka Mbinguni ili kuwanyakua watakatifu wake na kurudi kwake duniani ili kumhukumu Ibilisi kwa kupitia vita ya Harmagedoni ni mambo mawili tofauti. 
Baaba ya ile miaka mitatu na nusu ya kwanza katika ile Dhiki Kuu kuisha, na mara baada ya mauaji wa watakatifu kutoka kwa Mpinga Kristo, basi Bwana atashuka toka Mbingunini. Wakati huu, watakatifu ambao watakuwa wamelala katika makaburi yao na watakatifu ambao watakuwa wamestahimili katika kipindi cha Dhiki pasipo kuipokea alama ya Mnyama na hivyo kuilinda imani yao watafufuliwa na kuinuliwa angani na kisha kuonana na Bwana angani. Kuanzia wakati huo na kuendelea, watakatifu watakuwa wakati wote pamoja na Bwana. Wakati huu, Bwana hatashuka hapa duniani. Kwa nini? Kwa sababu mapigo ya mabakuli saba ambayo yatamhukumu Shetani na Mpinga Kristo yatakuwa bado hayajamiminwa hapa duniani. 
Hivyo, Mtume Paulo katika 1 Wathesalonike 4:17 alitueleza kwamba, “Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.” Watakatifu waliopambana na Mpinga Kristo na kisha kuuawa kama wafia-dini ili kuilinda imani yao watashiriki katika ufufuo wa kwanza, kisha watakutana na Bwana angani na wala si hapa duniani, kisha wataingia katika karamu ya harusi ya Mwana-kondoo huko Mbinguni pamoja na Yesu Kristo, ambaye amefanyika kuwa Bwana-harusi wao. 
Baada ya hili, Mungu atawaamuru malaika wake kuyamimina mapigo ya mabakuli saba yaliyojazwa ghadhabu ya Mungu, mapigo ambayo alikuwa ameyahifadhi kwa uvumilivu tangu wakati wa uumbaji, kwa ajili ya Mpinga Kristo na wafuasi wake, na wenye dhambi wote wa ulimwengu huu watakaokuwa wapo duniani. Hivyo, ulimwengu utakabiliana na mapigo makubwa sana ambayo hakuna mfano wake uliowahi kuonekana hapo kabla. Watakatifu watakaokutana na Bwana angani watakuwa wakimsifu Bwana angani kwa ajili ya mapigo ya mabakuli saba yatakayokuwa yakimiminwa hapa duniani. 
Baada ya kuwa wameshiriki katika ufufuo na unyakuo kupitia Bwana, basi watasimama katika bahari ya kioo iliyochangamana na moto ili kuisifu hukumu ya haki ambayo Mungu anaileta duniani. Hivo, watakatifu ambao waliuawa na kuwa wafia-dini na walioshiriki katika ufufuo na unyakuo wao kwa kupitia nguvu za Bwana watamsifu Bwana bila kukoma, watamsifu kwa ajili ya wokovu ambao amewapatia, na kwa hukumu yake kwa Mpinga Kristo na watumishi wake kutokana na nguvu zake kuu na zisizo na kikomo. 
Kila mtu hapa ulimwenguni atateseka sana wakati malaika watakapokuwa wakiyamimina mapigo yao, yaani kuanzia pigo la vidonda na majipu, pigo la bahari kugeuka na kuwa damu; pigo la bahari kugeuka na kuwa damu; pigo la maji kugeuka na kuwa damu; pigo la kuunguzwa na joto kali la jua; na pigo la giza na maumivu. Wakati malaika wa sita atakapolimimina bakuli lake katika ule mkubwa wa Frati, maji yake yatakauka, ili kuiandaa njia ya wafalme toka mashariki. Kutokana na pigo hili kutakuwa na njaa kubwa sana itakayoikumba dunia, njaa ambayo italeta mateso makubwa kwa wanadamu. Mapepo yatakuwa mengi sana, huku yakishawishi roho za watu kupitia Mpinga Kristo na nabii wa uongo. 
Kisha, roho za mashetani zitawashawishi wafalme wa duniani kwa ajili ya vita na kuwakusanya mahali panapoitwa Harmagedoni ili kupigana na Mungu Mwenyezi. Hapa ndipo mahali ambapo vita ya mwisho kati ya Shetani na Mungu itapiganwa. Lakini kwa kuwa Yesu ni Mungu Mwenyezi, atashuka toka angani akiwa ameketi katika farasi mweupe pamoja na jeshi lake, atamshinda shetani, na kisha kumtupa Mnyama katika ziwa liwakalo kwa moto na kibiriti (Ufunuo 19:11-21). Kwa kuwa hivi sasa Yesu Kristo ana nguvu kamili kama Bwana anayekuja mara ya pili, basi ataonekana hapa duniani ili kuuhukumu ulimwengu na kumwangamiza Mnyama. 
Kwa hiyo, tunapaswa kutambua kwamba wakati Yesu Kristo atakaposhuka toka Mbinguni wakati wa unyakuo wa watakatifu, hatashuka hadi hapa duniani, bali atakuja angani na kuwachukua watakatifu kwenda mahali alipo, atawaruhusu kukutana nao angani na kuwaingiza katika karamu ya harusi Mbinguni. Wakati Bwana atakaporudi hapa duniani, atafanya hivyo ili kumshinda Shetani na jeshi lake wanaosimama kinyume na Mungu, atawashinda kwa Neno lake lenye nguvu katika Vita ya Harmagedoni, atafanya hivyo ili kumtupa Ibilisi katika ziwa la moto na kibiriti, na kisha kuwaua wafuasi wake wote watakaokuwa wamesalia. Huu ndio ujio wa Bwana wa mara ya pili. Tunapaswa kuwa na ufahamu na imani sahihi ambayo inaweza kutofautisha kati ya kushuka kwa Bwana angani na ujio wake wa mara ya pili hapa duniani. 
Hata hivyo kuna watu wengi wanaofikiri kwamba Bwana atashuka moja kwa moja hapa duniani wakati unyakuo utakapotokea. Kwa kweli hiyo si sahihi. Unyakuo utakapotokea, Bwana hatakuja hapa duniani, bali atakuwepo angani. Kwa maneno mengine, atawainua na kuwapokea watakatifu angani. 
Kwa hiyo, unapaswa kuondokana na fikra kwamba Bwana atakuja tena hapa duniani wakati wa unyakuo, na badala yake unapaswa kwa kuzingatia Neno lililoandikwa, uanapswa kufahamu kwamba unyakuo wa watakatifu utatokea wakati malaika wa saba atakapolipiga tarumbeta lake. 
 

12) Je, “mkutano mkubwa ambao hakuna anayeweza kuuhesabu (Ufunuo 7:9)” una maanisha ni watakatifu walionyakuliwa?
 
Ndiyo, hiyo ni sahihi kabisa. Ufunuo 7:9 inaeleza, “Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao,” hapa tunaweza kuona kwamba kwa imani yao katika injili ya maji na Roho, idadi kubwa ya makutano miongoni mwa Wamataifa watapambana na kumshinda Mpinga Kristo, halafu wauawa na kuwa wafia-dini, kisha watashiriki katika ufufuo wa kwanza na kunyakuliwa. 
Ingawa katika siku hizi za mwisho Mpinga Kristo atacharuka pasipo kuhofia adhabu, basi tunaweza kuona kwamba katika nyakati hizo kutainuka idadi kubwa ya watu wanaoamini katika injili ya maji na Roho iliyotolewa na Mungu. Kwa hiyo, mkutano mkuu utatokea miongoni mwa Wamataifa, mkutano ambao ni mkubwa kiasi kuwa hakuna hata mmoja anayeweza kuuhesabu, huo utakuwa ni mkutano wa watu ambao wameokolewa toka katika dhambi kwa kuamini katika injili ya maji na Roho na kisha kupokea vifo vya kuwa wafia-dini kwa imani. 
Ufunuo 7:14 inasema, “Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe. Akaniambia, Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Wakati Dhiki Kuu ilipokuja hapa duniani, watu hawa waliokolewa toka katika dhambi kwa kuamini kwa mioyo yao yote katika injili ya maji na Roho iliyokuwa ikihubiriwa na Kanisa la Mungu. Hivyo waliuawa na kuwa wafia-dini, kwa kuwa hawakumwabudu Mpinga Kristo wala kuipokea alama ya Mnyama katika mikono yao ya kulia au katika vipaji vya nyuso zao, hivyo wakajiunga katika ufufuo wa watakatifu na unyakuo. Hii ndio maana wanasimama mbele ya kiti cha enzi na mbele ya Mwana-kondoo huku wakisifu; “Wakilia kwa sauti kuu wakisema, Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo!”
Hivyo, Mungu, si Mungu wa Wayahudi, bali ni Mungu pia wa Wamataifa. Kwa hiyo, Mungu atahakikisha kwamba wakati siku za Dhiki Kuu zitakapowadia, idadi kubwa ya Wamataifa toka mataifa mbalimbali, makabila, watu, na lugha mbalimbali wataiamini injili ya maji na Roho, watapokea ondoleo la dhambi, kisha watasimama miongoni mwa orodha ya wafia-dini. 
 

13) Mashahidi wawili wanafufuliwa na kunyakuliwa mbinguni baada ya kuukamilisha ushuhuda wao. Hii ina utofauti gani na kunyakuliwa kwa watakatifu kwa ujio wa Kristo mara ya pili? 
 
Kama nilivyoeleza kwa majibu yangu kwa swali la 2, mashahidi hawa wawili ni watumishi maalumu wa Mungu ambao atawainua toka kwa watu wa Israeli ili kuwaokoa Waisraeli. Kuna kazi muhimu ambayo ni lazima Mungu ataifanya kabla ya kuuangamiza ulimwengu huu, na kazi hiyo ni kuwaokoa watu wa Israeli toka katika dhambi na kuwafanya washiriki katika ufufuo wa kwanza na unyakuo. 
Katika Warumi 3:29-30 Mtume Paulo anasema, “Au je! Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Siye Mungu wa Mataifa pia? Naam, ni Mungu wa Mataifa pia; kama kwa kweli Mungu ni mmoja, atakayewahesabia haki wale waliotahiriwa katika imani, nao wale wasiotahiriwa atawahesabia haki kwa njia ya imani iyo hiyo.” Njia ya kuokolewa toka katika dhambi mbele za Mungu ni sawa kwa Wayahudi na kwa Wamataifa pia. Kwa Wayahudi na kwa Wamataifa pia, wokovu unawajia kwa njia ya imani tu katika injili ya maji na Roho. Ili waweze kuokolewa toka katika dhambi zao zote, basi Wayahudi ni lazima wampokee Yesu Kristo kuwa ni Mwokozi wao na waweze kuamini, yaani kama Wamataifa walivyoamini, kwamba Yesu Kristo alizichukua dhambi zao zote katika mwili wake kwa ubatizo wake, na kwamba alikufa Msalabani ili kuhukumiwa kwa ajili ya dhambi kwa niaba yao. 
Mungu anawatendea Wayahudi pamoja na Wamataifa sawia, na amewaruhusu kupata wokovu kwa njia ya imani. Hii ndio sababu Mungu aliwaruhusu mashahidi wake wawili kwa watu wa Kiyahudi wakati wa miaka mitatu na nusu ya kwanza ya ile Dhiki Kuu, na ndio sababu Mungu aliwaruhusu mashahidi hawa kuihubiri injili ya maji na Roho kwao. 
Sura ya 11 ya Ufunuo inaelezea juu ya mizeituni miwili na vinara viwili vya taa ambavyo vinahusianishwa na mashahidi hawa wawili. Mizeituni miwili ina maanisha ni watumishi wawili wa Mungu ambao Mungu atawaruhusu kwa ajili ya wokovu wa Waisraeli, na vinara viwili vya taa vina maanisha ni makanisa mawili ya Mungu, ambayo ni kwa ajili ya Waisraeli na kwa ajili ya Wamataifa. Kwa maneno mengine, Mungu atayaruhusu Makanisa yake mawili kwa pamoja kuihubiri injili ya maji na Roho kwa Waisraeli na Wamataifa katika kipindi cha miaka mitatu na nusu ya kwanza katika ile miaka ya Dhiki Kuu. 
Hivi sasa, Kanisa la Mungu linapatikana kati ya Waisraeli. Lakini wakati Mungu anapoiangalia mioyo yao na wakati wake utakapowadia, Mungu ataiandaa mioyo yao kulipokea Neno lake, atawainua watumishi wawili kwa ajili yao, na atawafanya wampokee Yesu Kristo kuwa ni Mwokozi wao. 
Hivyo, Mungu atawaokoa Waisraeli na Wayahudi katika wakati wa Dhiki Kuu. Pia ataruhusu mateso na mauaji ya wafia-dini kwa watakatifu waliozaliwa tena upya kwa Waisraeli na kwa Wamataifa pia. Ule ukweli kwamba mashahidi wawili watauawa na kuwa wafia-dini baada ya kuutimiza ushuhuda wao na kisha kufufuliwa na kunyakuliwa mbinguni kwa siku tatu na nusu—basi, kama ilivyotokea kwa mashahidi hawa, vivyo hivyo watumishi wa Mungu na watu wake miongoni mwa Wamataifa watapambana dhidi ya Mpinga Kristo, watauawa na kuwa wafia-dini, na hivyo watashiriki katika ufufuo wao na katika unyakuo. 
 

14) Ninaamini kwamba watakatifu watanyakuliwa kabla ya Dhiki Kuu. Lakini Biblia inaeleza mara nyingi juu ya watakatifu watakaokuwa wamebakia hapa duniani wakati wa Dhiki Kuu. Je, hao ndio wale waliokubaliana na ulimwengu, na ambao imani yao iligeuka na kuwa ya vuguvugu? 
 
Kwanza kabisa, unapaswa kutambua kwamba nadharia ya kunyakuliwa kabla ya dhiki unayoimani ni mafundisho ya uongo. Hii ndio sehemu ambayo Wakristo wengi wameielewa vibaya. Wanafikiri kwamba kwa kuwa watakatifu watakuwa wamekwisha nyakuliwa kabla ya Dhiki Kuu, basi wakati huo utakapowadia utawakuta wenye dhambi peke yao hapa duniani. Hata hivyo, tatizo ni kwamba Biblia inataja mara nyingi juu ya watakatifu ambao, walipokuwa hapa duniani wakati wa Dhiki Kuu, waliyashinda mateso kwa uvumilivu na kisha kuuawa kama wafia-dini. 
Hivyo, watu wengi wanafikiri kimakosa kwamba watakatifu hawa ambao wameachwa duniani na kisha kuteswa wakati wa Dhiki ndio wale ambao walikubaliana na ulimwengu na ambao imani yao ilikuwa ya vuguvugu. 
Watu wanaoshikilia mtazamo huu wanaishi katika hali ya kuchanganyikiwa kwa kuwa hawaufahamu wakati maalum wa unyakuo kama unavyoelezwa katika Neno la Mungu. Sasa, wakati hasa wa unyakuo ni lini? Paulo katika 2 Wathesalonike 2:1-4 anazungumza nasi kuhusu jambo hili kama ifuatavyo: “Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake, kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo. Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.”
“Mtu wa kuasi… mwana wa uharibifu” maana yake ni Mpinga Kristo ambaye atatokea katikati ya Dhiki Kuu. Kwa maneno mengine, Mpinga Kristo atatokea hapa ulimwenguni kabla ya unyakuo na atajiinua kana kwamba ni Mungu. Hivyo atafanyika sanamu yake na kuwalazimisha watu waiabudu na kumtumikia yeye. Ili kumfanya kila mtu kuwa chini ya utawala wake, basi Mpinga Kristo atawafanya watu kuipokea alama au jina la Mnyama katika mikono yao ya kuume au katika vipaji vya nyuso zao, na atamzuia yeyote asiyekuwa na alama hii kutonunua au kuuza chochote. 
Wakati Mnyama huyu atakapoonekana hapa ulimwenguni, watu wa ulimwengu huu watalazimishwa kuipokea alama iliyotengenezwa kwa jina lake au kwa namba ya jina lake. Kwa hiyo, yeyote ambaye jina lake halijaandikwa katika Kitabu cha Uzima tangu uumbaji ataishia kuipokea alama na kumwabudu Mnyama. 
Hata hivyo, kwa kuwa watakatifu ambao wamefanyika kuwa watu wa Mungu wana Roho Mtakatifu ndani ya mioyo yao, wao hawataweza kumwabudu kiumbe yeyote yule mbali ya Bwana Mungu wao kana kwamba ni Mungu. Hivyo, Roho Mtakatifu anayekaa ndani yao atawapa nguvu ya kupinga shuruti za Shetani na za Mpinga Kristo na nguvu ya kuilinda imani yao kwa kuwa wafia-dini. Pia Roho Mtakatifu atawapatia maneno ambayo kwa hayo wanaweza kusimama kinyume na maadui zao. 
Ufunuo 17:12-13 inatueleza kwamba, “Na zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi, ambao hawajapokea ufalme bado, lakini wapokea mamlaka kama wafalme muda wa saa moja pamoja na yule mnyama. Hawa wana shauri moja, nao wampa yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao.” Mpinga Kristo atapokea mamlaka ya kuwatesa watakatifu na kuyatawala mataifa ya ulimwenguni kwa kipindi kifupi tu. Hivyo, madai ya Mpinga Kristo ya kuipokea alama yake yatafuatiwa muda si mrefu na mauaji ya watakatifu ya kuwa wafia-dini. 
Kwa upande mwingine, Ufunuo 11:11-12, inatueleza kwamba, “Na baada ya siku hizo tatu u nusu, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama. Wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, Pandeni hata huku. Wakapanda mbinguni katika wingu, adui zao wakiwatazama.” Kutokana na ukweli huu, kwamba mashahidi wawili waliouawa kama wafia-dini walifufuliwa na kunyakuliwa baada ya siku tatu na nusu, basi tunaweza kuona kwamba kipindi kati ya mauaji yetu ya kuwa wafia-dini na kunyakuliwa kwetu si mbali sana pia. Mashahidi hawa wawili walinyakuliwa mara walipofufuliwa. Wakati Bwana atakaporudi, watakatifu waliouawa kama wafia-dini na watakatifu watakaokuwa hai ambao hawakuipokea alama ya Mnyama watafufuliwa wote, watanyakuliwa angani, kisha watamlaki Bwana angani. 
Hivyo, tunaweza kutambua kwamba kuonekana kwa Mpinga Kristo, mauaji ya watakatifu ya kufia-dini na kufufuliwa kwao, na unyakuo, vyote hivyo vinahusiana. Paulo na Yohana walituelezea kwa kina juu ya wakati wa unyakuo wa watakatifu. Watakatifu wote watakipitia kipindi cha miaka mitatu na nusu ya kwanza katika ile Dhiki Kuu. Kwa maneno mengine, watakatifu watakuwepo hapa duniani hadi mapigo ya matarumbeta saba yatakapoisha. 
Baada ya kuonekana kwa Mpinga Kristo, watakatifu wataingia katika kipindi cha pili cha miaka mitatu na nusu katika ile miaka ya Dhiki Kuu, na watakuwepo hapa duniani hadi pale watakapouawa na kuwa wafia-dini kwa kukataa kuipokea alama ya Mnyama. Hali tukilitambua hili, basi sisi sote tunapaswa kupokea malezi ya imani katika Kanisa la Mungu, yaani wakati huu wa sasa.